Sunday 29 July 2007

Ukaguzi wa magari nje wachefua wabunge

Ukaguzi wa magari nje wachefua wabunge
Halima Mlacha, Dodoma
HabariLeo; Saturday,July 28, 2007 @00:03
WABUNGE wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wale wa upinzani, jana walimtaka Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Basil Mramba, kufuta uamuzi wa kuteua mawakala maalumu wa kukagua magari nje ya nchi yanayoingia nchini.

Chini ya utaratibu huo, Shirika la Viwango Tanzania (TBS), limeteua mawakala maalumu wa kukagua magari nje ya nchi yanayoingia nchini.

Kwa sasa, tayari ipo sheria ya Kudhibiti Uingizwaji wa Magari Chakavu na Mamlaka ya Mapato (TRA), ndio wanaofanya ukaguzi huo na mwenye gari hulazimika kulipia ushuru zaidi kama gari lake ni la zaidi ya miaka 10.

Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Uwekezaji na Biashara, Abdallah Sumry (CCM), alisema kamati inaiona tenda hiyo ya ukaguzi wa magari nje, kama ni usumbufu kwa Watanzania na njia ya baadhi ya watu kujipatia kipato cha bure.

“Kamati inaona ukaguzi huu wa magari nje ya nchi yanayoingia Tanzania ni usumbufu kwa Watanzania na ni aina fulani ya watu kujipatia kipato bure tena cha fedha za kigeni kisichofaidisha nchi,” alisema mbunge huyo wa Mpanda Magharibi (CCM).

Alisema kwa sasa tayari ipo sheria ya Kudhibiti Uingizwaji wa Magari Chakavu na Mamlaka ya Mapato (TRA), ndio wanaofanya ukaguzi huo na mwenye gari hulazimika kulipia ushuru zaidi kama gari lake ni la zaidi ya miaka 10.

Alisema kamati hiyo inashauri ukaguzi huo usiendelee ili kutowabebesha mizigo mizito Watanzania wanaoagiza magari kutoka nje na kusisitiza juu ya umuhimu wa sheria hiyo iliyopitishwa bungeni kufanya kazi yake kama ilivyokusudiwa.


Naye Msemaji wa Kambi ya Upinzani, Lucy Owenya Viti Maalumu (Chadema), alisema mpango huo wa kuteua mawakala kutoka nchi za nje kwa ajili ya ukaguzi wa magari yanayoingia nchini, umepitwa na wakati.

Alisema hiyo ni kutokana na hatua ya Wizara ya Fedha kupitisha Sheria ndogo kwamba magari yenye umri zaidi ya miaka 10 lazima yatozwe ushuru mkubwa. “Kwa maana hiyo hakuna mtu atakayeingiza gari mbovu kutokana na kipengele hicho,” alisisitiza Owenya.

Alisema kambi hiyo inaona kuwa kitendo hicho ni njia ya kuwatafutia baadhi ya watu ulaji kwa jasho la Watanzania wanaoleta magari nchini, na alizitaja baadhi ya nchi ambazo TBS imewateua wakala wa kukagua magari hayo kuwa ni Dubai, Hong Kong, Thailand, Japan na Uingereza.

Naye Mbunge wa Solwa, Ahmed Ally Salum (CCM), alisema anasikitishwa na utaratibu huo ulioanzishwa kwani umewafaidisha wachache na kuwakandamiza zaidi Watanzania wanaojitahidi kujikwamua na umasikini.


“Hivi wakati gari inapigwa ushuru chakavu wewe unalikagua tena la nini, tunaomba Waziri Mramba uondoe tatizo hili kwani linamnufaisha tu aliyekuwa akiongoza mradi huu ambaye kwa sasa inasemekana amejenga nyumba yenye thamani ya dola za Marekani milioni 600,” alisema Salum.

Kwa upande wake, Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono (CCM), akichangia makadirio ya wizara hiyo, aliwataka Watanzania kubadilika na kuacha kununua malighafi kutoka nje ya nchi na badala yake watumie za ndani.

Alitolea mfano viti na kapeti la Bunge pamoja na suti za watu wengi waliovaa, kuwa ni malighafi kutoka nje hali inayochangia Shilingi ya Tanzania kushuka. “Wakoloni zamani walikuwa wakitumia malighafi za hapa kwetu na kutengeneza makochi, meza, lakini sasa hivi tunapenda vitu vya nje mpaka dawa ya mswaki,” alisema.

Naye Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo (Chadema), aliiomba serikali ianzishe mkakati wa kuinua wafanyabiashara tangu ngazi za chini kwa kuanzia na wafanyabiashara wadogo (wamachinga).

“Tusiache wale wafanyabiashara haramu kama vile wauza dawa za kulevya ndio baadaye waje waibuke kuwa wafanyabiashara wakubwa, lazima tujenge wafanyabiashara watakaojenga nchi hasa hawa wamachinga,” alisema Ndesamburo.

Naye Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Basil Mramba, akiwasilisha makadirio na matumizi ya fedha ya wizara yake, alisema katika kuimarisha viwanda na biashara nchini, wizara hiyo ina mpango wa kuanzisha miji au vitovu vya biashara pamoja na kuanzisha kituo cha kwanza cha kimataifa cha biashara kwa ajili ya kuwavutia wawekezaji.

Hata hivyo, Mramba alizitaka taasisi za fedha zenye kutoa masharti magumu kuacha tabia hiyo kwa kisingizio cha walengwa kutokopesheka badala yake zianze kutoa mikopo ili kuinua sekta ya viwanda na biashara nchini.


Pamoja na hayo aliwataka wananchi kuendeleza ujasiriamali na uzalendo kwa kutoa kipaumbele katika ununuzi wa bidhaa zinazozalishwa nchini ikiwa ni pamoja na serikali na taasisi kutoa zabuni kwa wazalendo.


Alisema sekta hiyo ya viwanda kwa sasa ina mafanikio makubwa kwani uchangiaji wake katika pato la taifa umeongezeka kutoka Sh bilioni 200.8 mwaka 2005 hadi Sh bilioni 218.1 mwaka jana.

Saturday 28 July 2007

Bunge linaongelea swala zima la TBS Saga

Napenda kuwataarifuni effort na juhudi za http://www.tbswtmuncovered.blogspot.com/ na wadau wote walioshiriki katika kupingana na swala hili, limewezesha kufanikisha hili swala mpaka katika ngazi ya juu ya kiserikali.

Tunawashukuru sana gazeti la mwananchi kwa ujumla, hususan juhudi za wahariri kupokea malalamiko yetu, hadi kufikia kuchapisha barua ya wazi kwa rais katika gazeti lao, na kuwezesha kulifikisha kwa wabunge na viongozi wa ngazi za juu ndani ya nchi. Hatimae linajadiliwa bungeni.

Juhudi zetu, hatimae tunategemewa kufanyiwa kazi, kwa vitendo na siyo MANENO matupu.



Wakereketwa..

Monday 2 July 2007

TBS - release Silly Statement!

It is unfortunate that, TBS are now in contrary contradicting themselves from their duly over due statement, and cleary put WTM utility on peculiar position. The bad news is that WTM Utility is clearly breaking every term of their contracts or well according to TBS.. Read more..

Where should I start ?

The big question is why TBS award a contract to a single entity, ie WTM Utility at the first place serving East London, what about other areas in London West, South and North, what about Leicester, Manchester Glasgow, and other major cities in UK. Which company/organization will be carrying out this exercise of inspection on TBS behalf ???

If TBS did not reach an agreement or reach a certain consensus with the MOT England at the first place, why going ahead with the ill thought exercise at the first place.

Quote from the statement
…and arrangements are underway to have a memorandum of understanding with MOT on vehicles tested for export to Tanzania…..

Unquote.



Lets be honest and frank on this matter. The whole saga surely should be considered either misconduct of duties or averting the cause of just duties. What I am trying to say is that all the individuals within the ranks of TBS and those in the decision makings should be held accountable to that effect.

Surely what it seems from their statement is that, They will go around the country, agreeing and sign contracts with every single garages, which seems to suit their TBS so called standards, Bad news to them is that there are 18000+ of them, they are all providing MOT certificates, surely it will be seen nuisance for them to provide TBS and MOT certificate of the similar standards??? Therefore conducting same checks/procedure and standards as that provided by TBS…This would be seen idiotic at the first place..

Secondly, you cannot compare Dubai/Sharjah with UK. Dubai/Sharjah is a federation of small countries called UAE, they are merely a cities not countries at all, and they are probably don’t have same procedures/standards as that provided by MOT and Europe in large.

Here are some facts to ponder:-

About Dubai
*Population 2.5Millions
*Area 83000+square kms
**Test Centres: 1

About Sharjah
*Area 400,339+ square kms
**Test Centres: 1

About London
*Population 7.2Millions
*Area 1579+ square kms
**Test Centres: 1000+


Looking at the facts above, TBS should have a prior knowledge of the readily available testing centres across the UK. Here is a smart Suggestion, In order to resolve the issue of talking/negotiating directly with individual test Centres, TBS should have contacted VOSA, a governing body which oversee the MOT.

Here is another advice, In UK there are private garages called , kwik-fit , posses garages across the country-providing MOT, why not talking to them, and avoid the complexity of negotiating with the Government, if that does not suit their appetite.

Conclusion

Looking at the statement, it seems TBS is trying to distance itself from the whole SAGA, by releasing silly statement, which is vague, unclear and confusing to anyone who understands.


The last thing is that, TBS is trying to tell poor WTM and fool us in general, According to their statement, WTM is surely breaking every term of their Contract.. Quote
... WTM Utility Services license clearly stipulates that its operation will be localized at East London....

Unquote.

Is TBS trying to tell the business Community it is illegal for WTM utility to inspect any vehicle from other part of London, or even surrounding cities. This statement is clearly a warning to WTM . YOUR IN A BREACH OF YOUR CONTRACT!

TBS mumechemsha!


**Test Centres: Following set of standards set by MOT-UK and TBS-Tanzania.
*All facts retrieved from Wikipedia

Sunday 24 June 2007

Watumishi wasiofuata maadili washughulikiwe - JK

007-06-24 09:57:17
Na Raymond Kaminyoge

Rais Jakaya Kikwete ameagiza watendaji wakuu, kuwashughulikia haraka watumishi wasiofuata maadili katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Rais Kikwete alisema hayo jana, Jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza katika kilele cha wiki ya utumishi.

Alisema watumishi wa umma wanalo jukumu la kuwapa huduma bora wananchi kwa kufuata maadili bila kuwabagua.

Alisema serikali itaendelea kupambana na uzembe kwa nguvu zake zote hadi utumishi wa umma utakapokuwa safi na uliotukuka.

Alisema utumishi wa umma umeshajiwekea kanuni na maadili ya kiutendaji ambayo watumishi wanayajua na kilichobakia ni kuyatekeleza kwa dhati katika kuwahudumia wananchi.

Alisema kuwashughulikia watumishi ambao hawafuati maadili kunahitaji viongozi wenye tabia ya kutowaonea aibu watumishi wasioyafuata.

Alisema watumishi wa umma wanatakiwa kubadilika kwa kutoa huduma bora kwa wananchi wakati serikali inaendelea kuboresha maslahi yao.

``Wakati serikali inaboresha maslahi na mazingira ya kufanyia kazi, watumishi warudishe fadhila hizi kwa kuwahudumia wananchi ambao wanatoa kodi ambazo zinawawezesha wao kulipwa mishahara`` alisema.

Aidha, aliwataka kuwa mstari wa mbele katika kupambana na rushwa ikizingatiwa kuwa utumishi wa umma ndiyo injini ya serikali katika kutekeleza majukumu yake.

``Kama mtumishi atagubikwa na rushwa, basi hali hii itaenea hata katika sekta nyingine binafsi ambazo zinautegemea utumishi wa umma kufanikisha kazi zake,`` alisema.

Rais Kikwete alisema kipimo cha mafanikio katika utumishi ni kupata majibu chanya katika masuala ya msingi yanayopima utekelezaji wa maboresho ya utumishi wa umma.

``Mnatakiwa kujiuliza, wananchi leo wanaheshimiwa na kuhudumiwa vizuri kuliko ilivyokuwa awali, au je, ni kwa kiasi gani watumishi wa umma wanazingatia maadili ya kazi zao na taaluma,``alisema.

Rais Kikwete aliongeza kuwa ni lazima utumishi wa umma uwe na mfumo wa mrejesho katika utoaji wa huduma toka kwa wananchi.

Alisema mrejesho huo utumiwe na asasi mbalimbali za serikali ili hatimaye utumike kufanya marekebisho katika maeneo ambayo huduma hazijaboreshwa.

``Lakini cha msingi zaidi tuwe na utaratibu na utamaduni wa kuwasikiliza wananchi, hili litachangia sana kwenye kupambana na watumishi wasio waadilifu, kupambana na rushwa na kutatua kero za wananchi,`` alisema.

Naye Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bi Hawa Ghasia alisema wiki ya utumishi wa umma imeenda sambamba na maonyesho ya taasisi za serikali.

Alisema jumla ya taasisi 77 zimeshiriki katika maonyesho ya mwaka huu ikilinganishwa na taasisi 27 ambazo zilishiriki mwaka jana.

``Kupitia maonyesho hayo kero nyingi zimeweza kutambuliwa kutoka kwa wadau ambazo ama tumezifanyia kazi au tunaendelea kutafuta majawabu kwa lengo la kuboresha huduma tunazozitoa kwa umma.

Alisema katika maonyesho yaliyopita, wadau wengi walilalamika kuwa kwa muda mrefu hawakuwa wamepandishwa vyeo.

Alisema baada ya malalamiko hao, ofisi yake ilishughulikia kero hizo na kupunguza tatizo hilo kwa asilimia kubwa.

Alisema ili kuboresha maadhimisho hayo na kuwawezesha wananchi wengi zaidi kufaidika na huduma za umma, miaka ijayo wizara hiyo itafanya maonyesho hayo kwa zamu katika mikoa mbalimbali hapa nchini.

Rais Kikwete aliwakabidhi washindi tuzo za utoaji wa huduma bora ambazo mshindi wa kwanza ni Wakala wa Mkemia wa Serikali, Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi na wizara ya Fedha ambayo ndiyo mshindi wa tatu.

* SOURCE: Nipashe

Saturday 16 June 2007

Barua ya Wazi kwa Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete

Mheshimiwa Rais, hii ni barua ya kuelezea malalamiko yetu watanzania juu ya utendaji wa kazi wa TBS (Tanzania Bureau Standard), kufuatia hatua iliyochukuliwa na TBS kuwazawadia WTM utility-http://www.wtmutilityservices.com/ zabuni ya ukaguzi wa magari yanayosafirishwa toka Uingereza kupelekwa Tanzania.

Muheshimiwa rais mengi ya malalamiko na maswali muhimu yameulizwa na wananchi, juu ya zoezi hili zima la ugawaji wa hii zabuni ambao umeenda kinyume na taratibu nzima za ugawaji wa zabuni hiyo. Baadhi ya sehemu ya hayo malalamiko yameelezwa wazi katika blog za wananchi, ambazo inaonyesha wazi malalamiko na kutoridhishwa kwao.

Kama utapata fursa pitia.

http://wemsas.blogspot.com/ Jumuiya ya Waswahili UK

http://www.tzcommunity.co.uk/ Jumuiya ya Watanzania UK

http://saidiyakubu.blogspot.com/2007/06/katika-taarifa-kwa-vyombo-vya-habari.html

http://tbswtmuncovered.blogspot.com/2007/06/tamko-rasmi-la-wtmtbs-uncovered.html


Muheshimiwa Rais, lazima ifahamike sisi wananchi hatuendani kinyume na taratibu za kudhibiti ubora wa magari au bidhaa nyengine zozote zinazoingizwa nchini toka nchi za nje, tunalopingana nalo ni ubora wa maamuzi ya TBS na ile kampuni iliyozawadiwa zabuni ya kufanya zoezi hilo, WTM utility

Muheshimiwa rais, kwa ufupi huku Uingereza, kipo kitengo maalum ambacho kinaangalia na kuongoza zoezi zima la ukaguzi wa magari madogo na makubwa(malori), kitengo hiki cha serikali kimeweka taratibu, njia na misingi kabambe ambayo kampuni ya WTM utility pekee haina au haiwezi kutimiza au kufikia viwango hivyo muhimu vilivyotolewa na VOSA-Vehicle and Operator Services Agency. Kitengo hiki maalum cha serikali ya Uingereza kinasimamia sehemu moja ya ubora wa magari yaliyo barabarani Uingereza kwa ujumla http://www.vosa.gov.uk/, au kwa jina maarufu inaitwa MOT.

Muheshimiwa rais, kitengo hiki cha serikali kinatoa vibali maalum kukagua magari kwa maelefu ya garage huko UK, ambayo idadi yake hadi kufikia mwaka jana ni 18300, ambavyo vinaendana na kanuni, ziliwekwa wazi kabisa kuhusiana na uangalizi wa magari yote Uingereza chini ya uangalizi wa kitengo hiki cha serikali- VOSA.

Swala la kujiuliza muheshimiwa Rais hawa WTM utility, wana garage moja au mbili katika nchi nzima ya Uingereza, na vile vile wanadai wanahimili mobile Units ambazo pia zitatumika katika zoezi hili la ukaguzi wa magari, hii peke yake inaenda kinyume na sheria na kanuni za sehemu ya ukaguzi wa magari, zaidi pitia hii tovotu inayoelezea wazi ya hizo kanuni za ubora wa sehemu ya ukaguzi. http://www.transportoffice.gov.uk/crt/motgaragesandtesters/applyingtobeanmottestcentre/premisesspecification.htm

Muheshimiwa rais, haya ni maswali muhimu ambayo tunakuomba sisi watanzania tunaoishi huku Uingereza, kuwauliza hawa TBS.

Je waliweza kuwasiliana na VOSA au ministry of Transport UK na jumuiya ya wafanyabiashara Uingereza na Tanzania, kuhusiana na zoezi hili zima la ukaguzi wa magari, kwa sababu ya kuuliza swala hili muheshimiwa rais ni kwa ajili ya kufahamu kama haya maamuzi yamepitia moja ya vipengele vyao vya kisheria katika kufikia maamuzi ya swala lolote linalohusiana na utungaji wa sheria ya viwango.

QUOTE

Preparation of Standards

Tanzania Standards are the national documents prepared through consensus of all interested parties i.e. consumers, producers buyers, research institutions, etc standard specify inter alia quality requirements for final products, sampling procedures, test methods, labelling, and good manufacturing practices… UNQOTE

Soma zaidi kupitia huo mtandao hapo chini..

http://www.tptanzania.co.tz/tbs_body.html

Je ni vipi WTM wataweza kuitumikia nchi nzima Uingereza, katika zoezi hili, hali ya kuwa garage ya zaidi 18000, ambazo zimesambaa Uingereza nzima, ambazo pia ndio zenye kufanya zoezi hilo hilo ambalo litafanywa na WTM utility, peke yake wenye garage 2 na mobile unit moja tu ?

Muheshimiwa Rais, sisi kama watanzania http://wemsas.blogspot.com/ tunaoishi huku UK, wengi wetu tunamadhumuni makubwa kabisa ya kuiendeleza nchi yetu katika sekta za kibiashara (import/export) na uwekezaji wa vitega uchumi ndani ya nchi. Yote haya ni makusudio ya kuweza kujisaidia na kujikwamua kiuchumi sisi wenyewe binafsi, ndugu, familia na watanzania walio chini kimapato, hii yote ni katika juhudi za kupigana vita na umaskini kama ilivyoolezewa katika ripoti ya mkukuta. http://www.povertymonitoring.go.tz/#

Muheshimiwa Rais baadhi ya maelezo ambayo yameelezwa katika ripoti hiyo ya mkukuta moja wapo ni kipengele cha tatu Governance and Accountability. Mwenendo wa TBS unaenda kinyume kabisa na vipengele vyote vilivyoelezwa katika ripoti hiyo muhimu ya kuondoa umaskini. Muheshimiwa Rais, TBS inakiuaka na kuzorotesha juhudi za MKUKUTA, kwa hiyo basi inarudisha juhudi za wananchi walio wengi katika kujikwamua na umaskini.

Baadhi ya hivyo vipengele kutoka ripoti ya 2006 ni kama ifuatavyo.

Quote

MKUKUTA CLUSTER III: Governance and Accountability

Assessment of broad outcomes

Assessment of cluster goals:

GOAL 1 Structures and systems of governance as well as the rule of law to be democratic, participatory,

representative, accountable, and inclusive

GOAL 2 Equitable allocation of public resources with corruption effectively addressed

GOAL 3 Effective public service framework in place to provide foundation for service delivery improvements

and poverty reduction

GOAL 4 Rights of the poor and vulnerable groups to be protected and promoted in the justice system

GOAL 5 Reduction of political and social exclusion and intolerance

GOAL 6 Improve personal and material security, reduce crime, and eliminate sexual abuse and domestic

violence

GOAL 7 National cultural identities enhanced and promoted

Unquote

Muheshimiwa rais tunakwamishwa vibaya na vyombo vya serikali, kama hiki cha TBS, mstaafu mwenyekiti wa TBS hapo awali, Mwakyembe aliwahi kusema “TBS siyo jeshi la ulinzi la Polisi” ambapo baadhi ya hotuba yake ilitolewa na gazeti binafsi kwenye tovotu hii http://www.ippmedia.com/ipp/guardian/2007/03/26/87090.html

Maombi ya Wafanyabiashara na Wananchi kwa ujumla.

Muheshimiwa rais, tunachokiomba sisi wananchi tunaoishi huku UK, tunakuomba utumie fursa yako, kwa kuuunda tume maalum ya kujitegemea kuchunguza swala hili, kama hivyo itagua vigumu muheshimiwa rais tunakuomba kupitia taasisi ya kuzuia rushwa http://www.tanzania.go.tz/pcb/rushwa/majukumu.html, kuweza kulifikisha swala hili na kuchunguzwa ipasavyo.

Kwa kumalizia.

Muheshimiwa Rais Nitakupa hadithi moja NASA - National Aeronautics and Space Administration ya Marekani, walitumia karibuni milioni moja dola, kwa kufanya utafiti wa kalamu itakayotumika kwenye SPACE shuttle.. Russia waliamua kutumia PENCIL. Je hii habari inalingana na hii ?? Ni kitu cha kujiuliza.

Ni mahisio yetu serikali ingetamka rasmi kupitia TBS, kwamba gari yoyote inayotoka Uingereza, ambayo itatumika Tanzania lazima iwe MOT certified, hilo lingeeleweka wazi kabisa, wengi tungelikaribisha na kulihimiza.

Shukrani Sana kwa kuchukua ujumbe wetu, ni mategemeo yetu tutapata maamuzi ya haraka. Na vile vile tungependa kutoa pongezi zetu za wazi zikufikie wewe pamoja na utawala wako katika kuweka uwazi katika maamuzi ya kiserikali yanayohusu wananchi au nchi nzima kwa ujumla.

Daima tutatumia fursa hii kupitia tovotu yako maalum kuleta mapendekezo au hoja zetu pale inapotubidi tufanye hivyo.

http://www.jakayakikwete.com/tanzania/pages/Ask-the-President

Mungu Ibariki Tanzania.

Shukran!

Thursday 14 June 2007

TBS is no police force, says Mwakyembe

Wakereketwa comments highlighted in red..

2007-03-26 09:00:25
By Patrick Kisembo

The government has called on the Tanzania Bureau of Standards (TBS) to contribute to the actualization of National Strategy for Growth and Poverty reduction (MKUKUTA) goal.

Je wafanyabiashara kama watumaji wa magari Tanzania toka UK hawamo katika hii programme nzima ya mkukuta.

Deputy Minister for Industry, Trade and Marketing, Hezekiah Chibulunje made the call on Friday, at a farewell party for outgoing TBS chief, Daimon Mwakyembe.

He urged TBS to adhere to the objectives of MKUKUTA in assisting small-scale industries.

The minister also urged TBS to ensure Tanzania does not become a dumping ground for counterfeit goods, which he said unfortunately have already flooded the country.

Hivi hawa TBS wanadhani mkakati mzima uliowekwa na Serikali kusitisha uingizaji wa magari madogo ambayo yana umri wa zaidi miaka kumi haitoshi ? Sisi huku UK tunaondesha magari ya 1995, na hakuna tatizo lolote alimradi, iko ndani ya vipimio vya MOT. na hawa TBS wanaelewa kuhusu counterfeit goods(mainly chinese imports), sijawahi kuona counterfeit cars, labda tuelemishane kwa hili...

`We are in a very competitive world. We need to produce quality goods which comply with the international standards for our survival,` he insisted. .. bado hatujaanza kuzalisha magari, until then msitunge standards ambazo hatunazo..

The outgoing TBS boss said he was grateful for the support he received from the government, members of the business community, hili linashaka TBS staff and other stakeholders during his tenure.

`I wouldn`t be here today if it were not for TBS executive council and the ministry responsible,` he said.

He called on for checks and balances so that TBS is not changed to some sort of a police unit such that stakeholders will run away whenever they see a vehicle lebelled TBS. It has become one, unfortunately.
`Let`s do the opposite and make people run towards us to seek advice or share information on TBS operations,` he insisted. Share information ?????

The Acting TBS DG, Charles Ekelege said the semi-autonomous body had recorded a number of achievements under Mwakyembe�s reign.

`In 1992 we had 528 standards but we now have 950 standards.Likewise we had 499 licenses but we now have 760,` he said.

Ekelege said TBS has started certifying standards of goods for other countries.

He said it was an indication that TBS was now recognized outside Tanzania�s borders.

TBS financial position had improved tremendously, he said.

`We used to collect 63m/- as an internal generation when Mwakyembe took over the office. However, we now collect 2.3bn/-,` the acting DG pointed out. , pesa zinaingia kwa wingi kama utaratibu ndio huu...